MADIWANI WANNE WA CHADEMA WAPIGWA MARUFUKU KUHUDHURIA VIKAO HADI JUNI 2019

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Siha, limewasimamisha madiwani wanne wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuhudhuria vikao vya baraza hilo hadi Juni mwaka 2019.

Madiwani hao wanadaiwa kuvunja kanuni ya 10 (d), kwa kuvua joho ambalo ni vazi maalumu lililochaguliwa na madiwani wa halmashauri hiyo kwa ajili ya mikutano ya baraza na hata walipotakiwa na mwenyekiti kuvaa joho hilo wanadaiwa kukaidi.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Valerian Juwal, amesema uamuzi huo una baraka za wajumbe wa baraza hilo.

Baadhi ya madiwani wanaodaiwa kusimamishwa ni pamoja na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Frank Tarimo, Diwani wa Kata ya Ivaeny, Elia Kiwia, Diwani wa Kata ya Kirua, Robert Mrisho na Diwani wa Viti Maalumu Witness Riwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527