LUGOLA ATAKA POLISI CHATO KUTOKUNYANYASA WANANCHI


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akitaka ufafanuzi kutoka kwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Chato, mkoani Geita, Alex Mukama (kulia), kuhusu uwepo wa pikipiki kituoni hapo wakati alishatoa agizo pikipiki ambazo hazina kesi mahakamani ziondolewe vituo vya polisi nchini. Kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Polisi Chato, Haruni Kasubo. Waziri Lugola alifika kituoni hapo mara baada ya kutoka kuhani msiba wa dada wa Rais Dkt. John Magufuli, wilayani humo leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akimpa maelekezo Mkuu wa Polisi Wilaya ya Chato, mkoani Geita, Alex Mukama (kushoto), kuhusu polisi wilayani humo wafanye kazi kwa weledi bila kunyanyasa wananchi. Waziri Lugola alifika Kituo cha Polisi Chato wilayani humo kusalimia pamoja na kupata taarifa ya utendaji kazi wa polisi, alipokua anatoka kuhani msiba wa dada wa Rais Dkt. John Magufuli, mjini Chato, leo. Kulia ni Mkuu wa Kituo hicho, Haruni Kasubo, na wapili kushoto, Diwani wa Kata ya Muungano, wilayani humo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akionyeshwa eneo la Kituo cha Polisi Chato na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Chato, mkoani Geita, Alex Mukama (kushoto). Waziri Lugola alifika Kituo cha Polisi Chato wilayani humo kusalimia pamoja na kupata taarifa ya utendaji kazi wa polisi, alipokua anatoka kuhani msiba wa dada wa Rais Dkt. John Magufuli, mjini Chato, leo. Katikati ni Mkuu wa Kituo hicho, Haruni Kasubo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527