LOWASSA KUZINDUA KAMPENI ZA UCHAGUZI CHADEMA MONDULI

Waziri Mkuu mstaafu ambaye pia in Mjumbe wa Kamati kuu Chadema, Edward Lowassa atazindua kampeni za uchaguzi mdogo wa Monduli, Jumatano Agosti 29, 2018.


Mwenyekiti wa Chadema Mkoa Arusha, Aman Golugwa amesema wamejipanga Jumatano Agosti 29 kuzindua kampeni kwa kishindo.


"Tutakuwa na viongozi kadhaa akiwamo Lowassa ambaye ni mbunge mstaafu wa Monduli na tuna uhakika wa ushindi tena Monduli," amesema.


Golugwa amesema chama hicho kinajua michezo michafu ambayo inaendelea kufanywa na CCM, lakini wanataka dunia ijue CCM haikubaliki tena.


"Kuna figisu figisu nyingi hata hizi za wagombea udiwani kupita bila kupingwa lakini wasifikiri Chadema itakufa," amesema.


Katika uchaguzi wa Monduli vyama vinane vinashiriki Chadema wamempitisha kugombea diwani wa Lepurko, Yonas Laizer.


Kata hiyo ndiyo anakotoka Kalanga ambaye pia alikuwa diwani wa kata hiyo hadi mwaka 2015 akiwa CCM na kujiunga na Chadema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527