DIAMOND PLATNUMZ AKABIDHI GARI KWA MUUZA MITUMBA SHINDANO LA NOGEWA USHINDE

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ambaye pia ndiye mkurugenzi wa WCB amemkabidhi gari mshindi wa shindano la Nogewa Ushinde lililokuwa likifanyika kwa mwezi mmoja sasa kupitia bidhaa za Diamond Karanga.


Mshindi huyo aliyejitambulisha kwa majina ya Bakari Saidi akisimulia kwa furaha amesema kuwa yeye ni muuza mitumba Ubungo jijini Dar es salaam na ameahidi kuendelea kutumia bidhaa hizo huku akidai kwamba gari hilo limemkomboa kiuchumi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527