BABU AFUNGA SMARTPHONE 11 KWENYE BAISKELI ILI ACHEZE ‘GAME’


Babu, Chen San Yuan, wa Taiwan, amefunga simu 11 kwenye baiskeli yake ili kila aendapo aweze kucheza michezo ya Pokemon iliyoko kwenye simu hizo.

Yuan, mwenye umri wa miaka 69 na anayeishi jiji la New Taipei, huzunguka na simu hizo kila mahali aendapo na akiingia mahali huzifungua kwenye baiskeli na kwenda nazo ili aweze kucheza wakati wowote.
Hulka hiyo ilianza mwaka 2016 wakati mjukuu wake alipomfundisha kucheza michezo hiyo ambayo imemjengea tabia hiyo ya kuutumia muda wake asipokuwa kazini kucheza michezo hiyo.
Licha ya kwamba simu hizo zimemgharimu Paundi 1,165 (Sh. mil. 3.3), bado anataka kununua simu nyingine zaidi ili zifike 15.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527