ALIYEIHAMA CHADEMA ASHINDA KWA KISHINDO UDIWANI CCM BUGARAMA KAHAMA

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka na ushindi katika uchaguzi wa marudio katika kata ya Bugalama iliyopo katika halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Kwenye uchaguzi huo uliofanyika Agosti 12,2018,Vyama vitatu vilisimamisha wagombea katika kata hiyo na mgombea wa CCM Izengo Josephat alitangazwa mshindi kwa kura 2137 akiwashinda wapinzani wake Stephano Izengo wa CHADEMA kwa kura 571 huku mgombea wa ACT wazalendo Jilala Seni akipata kura 32.

Uchaguzi huo wa marudio ulifanyika kufuatia aliyekuwa diwani wa CHADEMA Izengo Josephat kuhamia Chama Mha mapinduzi CCM na chama hicho kilimpa ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama hicho.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527