YANGA YAWEKA HADHARANI VIINGILIO VYA MCHEZO DHIDI YA GOR MAHIA

Uongozi wa klabu Yanga umetangaza viingilio vya mchezo wa mkondo wa pili dhidi ya Gor Mahia FC utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Julai 29 2018.


Kueleka mchezo huo wa Kombe la Shirikisho Afrika, Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten, amesema kuwa kiingilio cha chini kabisa kitakuwa ni shilingi 3000 pekee ambacho ni kwa jukwaa la mzunguko.


Katika jukwaa la VIP A kiingilio kitakuwa ni Tshs 10,000 huku VIP B na C kikiwa ni 7,000 pekee.


Yanga inaenda kucheza mchezo huo ikiwa inashika mkia kunako kundi D ikiwa na alama moja pekee iliyoipata baada ya suluhu tasa dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Taifa Dar.


Yanga inakutana na Gor Mahia ambayo iliwapa kichapo cha maana kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza jijini Nairobi kwenye Uwanja wa Moi Kasarani wa jumla ya mabao 4-0.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527