UFARANSA YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA DUNIA...YAIPA KICHAPO CHA 2-0 URUGUAY

Griezmann
Timu ya taifa ya Uruguay imeondolewa katika michuano ya Kombe la Dunia kwa kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Ufaransa.


Mchezo huo wa kwanza wa hatua ya robo fainali umemalizika kwa Ufaransa kujipatia mabao hayo kupitia kwa Raphale Varane na Antoine Griezman.


Matokeo hayo yanaifanya Ufansa kuipa tiketi Uruguay kuyaaga mashindano hayo ambayo ilitinga hatua hiyo baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ureno.

Baada ya mchezo huo, baadaye kutakuwa na mechi nyingine baina ya Brazil na Ujerumani kuanzia saa 3 kamili usiku huu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527