RAIS WA TFF AZUNGUMZIA UTEUZI WA RAIS MAGUFULI WANA MICHEZO WATATU


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amewapongeza wanamichezo watatu walioteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kushika nyadhifa mbalimbali.

Wanamichezo waliopata nafasi hizo ni Mussa Ramadhan Sima aliyeteuliwa kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Mazingira, Athuman Kihamia aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi katika Tume ya Uchaguzi (NEC) na Ramadhan Kailima aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Aidha, Rais Karia amesema kwa niaba ya TFF anawapongeza wanamichezo hao kwa nafasi zao mpya walizoteuliwa huku akidai anaamini kwa uchapakazi wao hawatamuangusha Rais Magufuli.

"Kwa niaba ya TFF nawapongeza wanamichezo wenzetu Kihamia ,Sima na Kailima kwa uteuzi wa nafasi zao mpya na nawatakia kila la heri kwenye nafasi zao", amesema Karia.

Kihamia yupo kwenye Kamati ya Ajira ya TFF wakati Sima ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira Wa Miguu Mkoa wa Singida.
Chanzo- EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post