Picha : JINSI MASHABIKI WA CROATIA WALIVYOSHEREHEA USIKU KUCHA KUWAPA KICHAPO ENGLAND

Mashabiki wakisherehekea Zagreb

Mashabiki wa Croatia walisherehekea usiku kucha baada ya taifa lao kuwaondoa England kutoka kwa michuano ya Kombe la Dunia Urusi na kufuzu kwa fainali kwa mara yao ya kwanza kabisa, England waliomboleza.

Croatia walipata ushindi wa 2-1 baada ya mechi kumalizika sare ya 1-1 muda wa ziada.

Mashabiki walijaza uwanja ulio katikati mwa mji mkuu wa Croatia wa Zagreb wakiimba na kupeperusha bendera za taifa hilo. Baadhi walijitumbukiza hadi kwenye chemchemi za maji zinazopamba uwanja huo.


Mabao yalivyofungwa

Kieran Trippier dakika ya 5 Croatia 0-1 England

Ivan Perisic dakika ya 68 Croatia 1-1 England

Mario Mandzukic dakika ya 109 Croatia 2-1 England

Croatia ni taifa la watu milioni nne hivi na ni moja ya mataifa yenye idadi ndogo sana ya watu kuwahi kufika fainali Kombe la Dunia. 

Watakutana na Ufaransa katika uwanja wa Luzhniki mjini Moscow Jumapili kwa fainali saa tatu usiku saa za Afrika Mashariki.

England watakutana na Ubelgiji mechi ya kuamua atakayemaliza nafasi ya tatu, mechi ambayo itachezewa mjini St Petersburg.

Kwa Croatia kukiwa kicheko na shangwe, kwa raia wa England kulienda masikitiko, huzuni na majonzi.
Mashabiki wakisherehekea ZagrebMashabiki wengi walijitokeza ZagrebMashabiki wakicheza kwenye maji kusherehekea katikati mwa mji wao mkuu ZagrebRais wa Croatia Kolinda Grabar-Kitarovic (kushoto) alimpa waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May jezi ya taifa hilo wakati wa mkutano mkuu wa Nato mjini Brussels, UbelgijiKiungo wa kati wa Croatia Luka Modric (kati) akiwa na Mario Mandzukic (kulia) wakisherehekea Luzhiniki, MoscowShabiki huyu kwa jina Daniel alisherehekea kwa kinywaji, na aliambia BBC kwamba "ushindi huo ni mkubwa mno" kwa taifa hilo ndogo

Hali ilivyokuwa kwa England:

Walianza kwa matumaini baada ya bao kufungwa dakika za kwanza lakini baadaye wakavunjwa moyo.
Ndoto kwisha: Mashabiki wakifarijiana katika bustani maarufu ya Hyde Park jijini LondonShabiki mdogo wa England akiliwazwa Castlefield Bowl, Manchester

Katika bustani ya Hyde Park, London, takriban mashabiki 30,000 walifika kutazama England wakicheza nusufainali, mkusanyiko mkubwa wa watu London kutazama mchezo wa kandanda tangu Euro 96. 
Shabiki huyu labda alizidi katika kusherehekea kabla ya mechi UrusiShabiki wa England akisherehekea karibu na shabiki wa Croatia kabla ya mechi UrusiMaelfu ya mashabiki Hyde Park kabla ya mechi kumalizikaWakati wa muda wa ziada Hyde ParkMashabiki wa England wakitokwa na machozi ManchesterManchester wakisherehekea baada ya England kufunga bao la kwanzaMashabiki wakitokwa na machozi Brighton BeachMashabiki waliovalia barakoa za Harry Brighton BeachShabiki wa England, Hyde ParkMashabiki walivyokuwa wakisherehekea awali Nottingham CastleLily Harkin mwenye miaka minane alikuwa ameandika mgongoni mwa Cole Bryceland, Nottingham kwa matumaini, 'Kombe linarejea nyumbani', lakini baadaye 'England walirejea nyumbani' bila kombeRoho mkononi Millennium Square, LeedsMasikitiko Hyde Park

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527