LUGOLA AFUNGUKA GUMZO LA SUTI ZAKE ZENYE MIFUKO YA BENDERA

Baada ya suti za Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, kuwa gumzo kwenye mitandao mbalimbali, mwenyewe amefunguka na kufafanua juu ya suala hilo.

Kwa muda sasa, tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo, Lugola amekuwa akivaa suti zenye bendera ya Tanzania kwenye mifuko hali ambayo imesababisha mijadala kwenye mitandao ya kijamii.


Akizungumza na Michuzi, Lugola alisema anazo suti nyingi za aina hiyo na ni yeye mwenyewe aliyeamua zifanane kwa mwonekano.


Baadhi ya wachangiaji kwenye mitandao ya kijamii wamekuwa wakihoji iweje Waziri avae suti moja muda mrefu wakidhani kuwa amekuwa akiirudia.


Lakini mwenyewe jana alijibu na kueleza kuwa suti hizo ambazo ameziita kuwa ni za aina yake, anazo nyingi lakini ameamua zote zifanane.


“Hata ninapobadilisha suti hizi hakuna anayeweza kujua kwa sababu zote zimefanana,” alisema.


Mwonekano wa suti hizo umefanya watu wengine kuzishangaa kutokana na mifuko ya shati kutengenezwa kwa bendera ya taifa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527