CHELSEA YATANGAZA KOCHA MPYA

Siku moja baada ya club ya Chelsea kutangaza kuwa wamemfuta kazi kocha wao Antonio Conte baada ya kudumu nae kwa miaka miwili akiwapa mataji ya EPL na Kombe la FA.
Leo club ya Chelsea imemtangaza rasmi kocha wa zamani wa Napoli Maurizio Sarrikuwa kocha wao mpya kwa mkataba wa miaka mitatu, Sarri anajiunga na Chelsea baada ya kuitumikia Napoli kwa miaka mitatu.
Sarri nafasi yake katika club ya Napoli ilitangazwa mapema kuchukuliwa na Carlo Ancelotti “Najisikia fahari kujiunga na Chelsea na kuja kufanya kazi premier League, najisikia fahari kuanza kazi na kukutana na wachezaji Jumatatu”, Maurizio Sarri

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527