Breaking : MBUNGE MWINGINE WA CHADEMA AJIUZULU NA KUHAMIA CCM

Julius Kalanga aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Monduli kupitia Chadema amejiuzulu nafasi zake zote ikiwemo Ubunge na kuhamia CCM usiku wa kuamkia leo.



Katika sababu mojawapo ya kujiuzulu aliyoieleza,amesema ni Kuunga mkono juhudi kubwa za kuleta maendeleo zinazofanywa na Rais Dkt John Pombe Magufuli.

"Siwezi kuwa sehemu ya kukwamisha maendeleo ya wananchi wa Monduli kwa kupinga kila kitu. Ubunge si tatizo kwangu naweza kuwa mkulima au mfugaji ila si kuwa kikwazo," amesema Kalanga


Hapo pichani alikuwa akitambulishwa rasmi usiku na Msemaji wa chama cha CCM,Ndugu Pole.


Kufuatia uamuzi huo jimbo la Monduli liko wazi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527