MKUU WA JESHI LA POLISI 'IGP' AJIUZULU...RAIS ARIDHIA


Rais wa Gambia, Adama Barrow

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Gambia amelazimika kujiuzulu baada ya watu watatu kuuwawa mapema wiki hii katika eneo la Faraba Banta, kusini mwa mji mkuu wa nchi hiyo Banjul, kufuatia polisi kuwafyatulia risasi waandamanaji.

Wakazi wa mji huo walikusanyika na kuandamana kupinga uchimbaji wa mchanga ambao umekua ukitishia mazingira na mashamba yao ya mchele.

Barua ya kujiuzulu ya Landing Kinteh ilikubaliwa na Rais Adama Barrow jana Alhamisi wiki hii baada ya kukosolewa na upinzani kufuatia vurugu za Faraba Banta. Hata hivyo amedai hakuwaamrisha polisi kuwafyatulia risasi waandamanaji.

Rais Adama Barrow anatarajia kuzuru mji huo wa Faraba Banta leo ili kukutana na familia za waathirika ambapo pia shughuli za uchimbaji mchanga zimesimamishwa kwa muda.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527