PROF. MWANDOSYA : SUGU UMEHITIMU CHUO CHA UANASIASA

Waziri wa serikali ya awamu ya nne Prof. Mark Mwandosya ameingia katika Orodha ya watu walioonesha furaha yao baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi kuachiliwa jana kutoka gerezani ambapo alihukumiwa kifungo cha miezi mitano.


Prof. Mwandosya ameandika katika ukurasa wake wa twitter; “Nikimpa hongera Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi kwa kuhitimu Chuo cha Uanasiasa, gereza la Ruanda, Mbeya. Kutofautiana vyama, itikadi na misimamo kusilete uhasama na uadui. Mungu Ibariki Tanzania.”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527