PIUS MSEKWA APONGEZA UTENDAJI WA RAIS MAGUFULI

Spika wa Bunge mstaafu, Mhe. Pius Msekwa amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli anafanya kazi vizuri katika kuiletea nchi maendeleo hasa kwa kulinda na kusimamia rasilimali .

Msekwa alisema hayo jana katika mahojiano na shirika moja la utangazaji la kimataifa yaliyofanyika Ukerewe, mkoani Mwanza.

"Mwenye macho haambiwi tazama, yanayofanywa na Rais Magufuli yanaonekana wazi hata yanatoka kwenye vyombo vya habari badala ya kubaki kwenye kumbukumbu za serikali", alisema Msekwa.

Kuhusu demokrasia nchini, Msekwa amesema kuwa hali ya demokrasia nchini inaridhisha kwani viongozi muda wao wa kukaa madarakani ukiisha wanaondoka. Wanaominya demokrasia ni wale wanaong'ang'ania madarakani baada ya kipindi chao kuisha, jambo ambalo kwa Serikali ya Tanzania halipo. Tangu Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani mambo mengi yamebadilika na kuwa bora zaidi. Mfano, nidhamu ya watumishi na uwajibikaji serikalini imeongezeka na hivyo ukiritimba na urasimu umepungua.

Huduma za Afya zimeboreshwa kwa kujenga na kukarabati hospitali, zahanati na vituo vya afya. Hii pia ni pamoja na upatikanaji wa dawa hospitalini kupitia bohari ya dawa ya serikali (MSD). 

Kwa kujali afya za Watanzania, Serikali imeongeza bajeti ya dawa kutoka bilioni 39 hadi bilioni 268, jambo ambalo limefafanya upatikanaji wa dawa kuongezeka.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527