BASI LAUA WATU 22 BAADA YA KUPARAMIA TINGATINGA

Takribani watu 22 wakiwemo watoto watatu wamefariki kwenye ajali ya basi kaskazini mwa Uganda kwa mujibu wa polisi.

Basi hilo liligonga tingatinga ambayo ilikuwa ikiendeshwa bila ya taa usiku kwa mujibu wa msemaji wa polisi Emilian Kayima ambaye aliongea na AFP.

Ajali hiyo ilitokea Ijumaa usiku huko Kiryandongo karibu kilomita 220 kaskazini mwa mji mkuu Kampala.

Baadhi ya vyombo vya habari vilisema kuwa watu waliofariki dunia walikuwa zaidi ya 30.

Uganda ina kati ya rekodi mbaya zaidi za usalama wa barabara. Zaidi ya watu 9,500 walifariki kwenye ajali za barabarani nchini humo kati ya mwaka 2015 na 2017 kwa mujibu wa takwimu rasmi.
Chanzo- BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527