WATOTO WAWILI WAFA MAJI WAKICHEZA KWENYE BWAWA TINDE SHINYANGA


Watoto wawili wenye umri wa mwaka mmoja wamefariki dunia baada ya kuzama katika bwawa lililopo katika katika kitongoji cha Mwandu,kijiji cha Buchama kata ya Tinde,tarafa ya Itwangi wilaya na mkoa wa shinyanga. 

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Simon Haule amesema tukio hilo limetokea Jumapili Aprili mosi,2018  asubuhi ambapo watoto hao waligundulika wakiwa wamekufa maji baada ya kuzama ndani ya bwawa la maji wakiwa wanacheza ndani ya bwawa hilo. 

Amesema watoto hao wawili ambao ni wa familia tofauti ni Sliva Mhoja mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi nane mkazi na Odisia Lugangula mwenye umri wa mwaka na miezi tisa wakazi wa Buchama. 

Kamanda Haule amekitaja chanzo cha tukio hilo kuwa ni watoto kucheza kwenye bwawa na kisha kuzama. 

Amesema miili ya marehemu imefanyiwa uchunguzi na mganga wa serikali na kisha kukabidhiwa kwa ndugu kwa mazishi. 

Kamanda Haule anawaasa wazazi, walezi na ndugu kuwa karibu sana na watoto wadogo hasa kufuatia mvua kubwa za masika zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali mkoani Shinyanga na hivyo kusababisha kuwepo kwa mabwawa mengi ambayo ni hatari kwa watoto wadogo wanaocheza maeneo hayo au kuogelea.

Na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527