RAIS MAGUFULI AITANGAZA DODOMA KUWA JIJI JIPYA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Aprili 26, 2018 ameupandisha hadhi mji wa Dodoma na kuwa jiji, huku akimtaja Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma wa sasa kuwa Mkurugenzi wa Jiji hilo jipya.

Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo wakati akihutubia wananchi walioweza kujitokeza katika viwanja vya Jamhuri vilivyopo Dodoma ambapo ndipo zilipofanyikia sherehe za miaka 54 ya Muungano kitaifa.

"Azma ya serikali kuhamia Dodoma ipo pale pale hakuna kurudi nyuma na tayari zaidi ya watumishi 3800 wameshahamia na mimi kama nilivyo ahidi mwaka huu nahamia Dodoma. Dodoma ndio makao makuu kwa hiyo kuanzia leo kwa mamlaka mliyonipa watanzania Dodoma ni Jiji", amesema Dkt. Magufuli.

Pamoja na hayo, Dkt. Magufuli ameendelea kwa kusema "kwa hiyo maandalizi yote ya kisheria yaanze kutumika katika jiji hili jipya na hili litakuwa Jiji la pekee yake kwasababu lipo kati ya Tanzania".

Kwa upande mwingine, Dkt. Magufuli amewahakikishia wananchi wa Tanzania kuwa wako safi bila ya kujali vyama vyao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527