FATMA KARUME NDIYO MRITHI WA TUNDU LISSU...ACHAGULIWA KUWA RAIS TLS

Wakili wa kujitegemea, Fatma Karume amechaguliwa kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Lawyers Society – TLS), akichukua mikoba ya aliyekuwa Rais wa Chama hicho, Tundu Lissu baada ya muda wake kumalizika.


Katika uchaguzi huo, Dkt. Rugemeleza Nshala amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa chama hicho.


Aidha, Ndugu Omar Shaaban amechaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar Lawyers Society.


Kwa mujibu wa katiba ya Chama hicho, Uongozi wa TLS hudumu kwa kipindi cha mwaka mmoja tu, na baada ya hapo viongozi wengine huchaguliwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527