ZARI THE BOSS LADY ATUA BONGO...ATOA NENO AKISAINI MKATABA MNONO

Mpenzi wa zamani wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Zarinah Hassan maarufu Zari The Boss Lady ametua nchini Tanzania kwa ajili ya kusaini mkataba wa ubalozi wa kampuni ya Kedz Tanzania inayojihusisha na utengenezaji wa pampasi.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika leo Jumatano Machi 28, 2018 katika Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam, Zari ambaye ni mama wa watoto watano amesema anashukuru kupata mkataba na kampuni hiyo.

Hata hivyo, kiu ya wanahabari ilikuwa kusikia akizungumzia uhusiano wake uliovunjika lakini alikwepa swali hilo akidai kuwa siyo  kilichomleta.

“Unajua hii ni kazi na haihusiani kabisa na masuala ya familia, hivyo nisingependa kulizungumzia hilo leo,” alifafanua.

Zari alitangaza kuachana na mwanamuziki Diamond Platnumz Februari 14, 2018 kupitia mtandao wa Instagram.

Wiki mbili baadaye akihojiwa na Kituo cha BBC Swahili, Zari amesema ameamua kuachana na Diamond kutokana na sababu mbalimbali moja ikiwa ni kushikana hadharani na mwigizaji Wema Sepetu.

Na Nasra Abdallah, Mwananchi


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527