UGONJWA HATARI 'DENGUE' WATUA TENA TANZANIA

Wizara ya Afya, Jinsia, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto imethibitisha kulipuka tena kwa ugonjwa wa Dengue ambao uliwahi kuibuka nchini na kuua baadhi ya watu.


Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv , msemaji wa Wizara ya Afya Nsachris Mwamwaja, amesema ni kweli ugonjwa huo umeripotiwa kuibuka tena, na taarifa kamili inatarajiwa kutolewa leo mchana na Waziri Ummy Mwalimu.

“Na kweli Katibu Mkuu aliitoa, lakini rasmi tutaoa wakati wowote leo, kuna shughuli ambayo ataifanya Waziri kwa hiyo kuna uwezekano akatoa taarifa hiyo kwa sababu imeshandaliwa”, amesema Bwana Mwamwaja.

Ugonjwa huo ambao unasababishwa nakirusi ambacho kinaenezwa na mbu wa aina ya Aedes., husababisha homa kali na hatimaye kifo, hivyo wananchi wanatakiwa kuwa makini na kutumia vyandarua wakati wa kulala, na kuepuka kukaa sehemu zenye mbu.
Chanzo- EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527