RAIS MAGUFULI KESHO KUFUNGUA BARABARA YA ISAKA - LUSAUNGA NA KIWANDA CHA KAHAMA OIL MILL


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kesho Jumamosi Machi 10,2018 atafanya ziara ya siku moja mkoani Shinyanga.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo, Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Zainab Telack amesema rais Magufuli atafanya ziara yake wilayani Kahama.

Amesema akiwa wilayani Kahama,kesho mchana Rais Magufuli atazindua barabara ya kiwango cha lami ya kutoka Isaka kwenda Lusaunga Ushirombo na kufungua kiwanda cha Kahama Oil Mill.

Amesema mheshimiwa rais pia atafanya mkutano wa hadhara kuzungumza na wananchi wilayani Kahama.

Na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527