MWANDISHI WA HABARI MTANZANIA ALIYEKIMBILIA FINLAND ASISITIZA KUPATA VITISHO


Mwandishi wa habari Ansbert Ngurumo ameijibu Serikali huku akisisitiza kupata vitisho, ikiwamo kutishiwa maisha kutokana na namna alivyowakosoa viongozi.

Majibu ya Ngurumo yametokana na maelezo ya Serikali kwamba madai ya mwandishi huyo si ya kweli na yamejaa usanii.

Ngurumo ambaye kwa sasa amepewa hifadhi nchini Finland, amedai kwamba Serikali haina rekodi nzuri juu ya watu wanaofuatiliwa na kutekwa ndiyo maana haijui hata Azory Gwanda na Ben Saanane waliko.

Amehoji kama maelezo yake ni usanii wanaotenda maovu ya kuteka na kutesa watu ndani ya nchi, inakuwaje Serikali isijue ni akina nani?

Ngurumo amesema wasamaria ndiyo waliomsaidia kutoroka na kuzijua mbinu za watu waliokuwa wakitaka kumdhulu, hasa katika mikoa ya Mwanza, Kagera na Dar es Salaam ikiwamo kuyatambua magari waliyokuwa wakiyatumia kumfuatilia.

Amesema mbali na kutoa taarifa kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter Oktoba 3, 2017, hakutaka tena kupiga kelele na badala yake aliendelea kupambana kimyakimya, kujilinda na kumulika wabaya wake akiwa mbali.

Na Aurea Simtowe,Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527