MAHAKAMA YAKUBALI HOJA TATU KESI YA BABU SEYA...IMO YA NGUVU ZA KIUME


Mahakama ya Afrika ya Haki za Binaadamu imekubali hoja 3 kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu katika kesi ya Babu Seya ikiwemo hoja ya Nguza Viking kutaka apimwe nguvu za kiume.

Akisoma hukumu kwa niaba ya majaji wenzake, Jaji Gerard Niyungeko aliainisha kwamba kati ya haki zilizokiukwa wakati wa mwenendo wa kesi hiyo ni ombi la Nguza Viking kupimwa kitabibu ili kuthibitisha kama hakuwa na nguvu za kiume na hivyo asingeweza kufanya vitendo vya ubakaji.

Mahakama hiyo imekubali pia hoja kwamba Viking (maarufu kama Babu Seya) na mwanaye, Johnson Nguza (maarufu kama Papii Kocha) hawakupata maelezo ya mashahidi wala fursa ya kuwahoji walotoa ushahidi ili kuthibitisha makosa.

Hata hivyo, hoja nyingine mbalimbali ziliwekwa kando ikiwemo hoja ya watuhumiwa hao kutolewa gerezani, huku mahakama ikisema kwamba tayari wameshatolewa kwa msamaha wa Rais John Magufuli.


Na Mussa Juma. Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527