BASI LAGONGANA NA HIACHE NA KUUA WATU WATANO MORO

Watu watano wamefariki dunia katika ajali iliyohusisha basi la kampuni ya New Force lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Tunduma mkoani Mbeya.


Ajali imetokea leo Machi 4,2018 eneo la Rungemba barabara ya Morogoro- Iringa.


Basi hilo limegongana na gari dogo aina ya Toyota Hiace lililokuwa likitokea Mlali wilayani Mvomero kwenda mjini Morogoro.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amethibitisha ajali hiyo akisema taarifa zaidi zitatolewa baadaye


Watu walioshuhudia ajali hiyo wameeleza chanzo ni uzembe wa dereva wa Hiace aliyekuwa akijaribu kulipita gari lililokuwa mbele yake, hivyo alikutana na basi la New Force lililokuwa katika njia yake.


Hiace ndilo lililoharibika zaidi katika ajali hiyo.


Na Amina Juma -Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527