Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Nyakoro Sirro, leo amefika kwenye msiba wa aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi juzi Ijumaa eneo la Mkwajuni, Kinondoni, Dar. Msiba huo upo nyumbani kwao Akwilina maeneo ya Mbezi jijini Dar es salaama.