TRUMP : KIBONYEZO CHANGU CHA NYUKLIA NI KIKUBWA NA KINA NGUVU KULIKO CHA KIM

Rais wa Marekani Donald Trump amejigamba kuwa kibonyezo chake cha silaha za nyuklia ni kikubwa na kilicho na nguvu zaidi kuliko kile cha kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jon-un.

Ujumbe wa Twitter wa Trump ndiyo wa hivi punde wakati ya majibizano kati ya viongozi wa mataifa hayo mawili yaliyo na silaha za nyukilia.

Mapema wiki hii Kim alionya kuwa kibonyezo chake cha nyuklia kawaida kiko kwenye meza yake.

Korea Kaskazini inadai kuwa ina silaha za nyulia na inaweza kuishambulia Marekani huku wadadisi wakisema kuwa ikiwa Korea Kaskazini ina silaha za nyulia haibainiki ikiwa ina teknolojia ya kuzitumia.

Kando na kuitishia Marekani, ujumbe wa mwaka mpya wa Kim pia uliwashangaza wengi wakati alisema kuwa alikuwa aayari kwa mazungumzo na Korea Kusini na ange[penda kuituma timu kwa mashindano ya olimpiki ya msimu wa baridi nchini Korea Kusini mwezi ujao.
Chanzo-BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527