Maajabu haya : WANAFUNZI WOTE WA SHULE YA SEKONDARI NJOMBE WAPATA DARAJA SIFURI (0)...WAZIRI ACHARUKA

Naibu Waziri Ofisi ya Rais –Tamisemi, Joseph Kakunda ameagiza mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Njombe kufanya uchunguzi wa matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Viziwi Njombe.


Katika matokeo yaliyotangazwa jana Jumanne Januari 30,2018 na Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), shule hiyo katika matokeo ya mtihani uliofanyika Oktoba na Novemba mwaka jana watahiniwa wote 21 wamepata daraja sifuri (0).

Naibu Waziri Kakunda ametoa agizo la kufanyika uchunguzi leo Jumatano Januari 31,2018 bungeni alipojibu swali la mbunge wa Buyungu (Chadema), Samson Bilago.


Bilago alitaka kujua ni kwa nini shule za wanafunzi wenye mahitaji maalumu zinafanya vibaya kwenye mitihani.

Akizungumzia hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema walimu waliosoma elimu maalumu watapata ajira bila kikwazo cha kusubiri.

Mkuchika amesema wanasubiri kupelekewa orodha ya walimu hao.

Alikuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini aliyetoa mfano wa shule ya Viziwi Njombe ya wanafunzi wa mahitaji maalumu iliyofanya vibaya katika matokeo ya mitihani ya kidato cha nne akisema ni kutokana na kukosa walimu hao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527