NYUMBA YA MBUNGE WA CHADEMA SILINDE DAVID KUCHOMWA MOTO

Mbunge wa Momba (Chadema), David Silinde amesema siku akitangaza kukihama chama hicho wananchi wajitokeze kuchoma moto nyumba yake pamoja na mali zake zinazofahamika.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Desemba 15, muda mfupi baada ya kusambaa kwa taarifa za kutaka kukihama chama hicho kikuu cha upinzani nchini, Silinde amesema ubunge wa jimbo hilo aliutafuta kwa gharama kubwa.

“Kinachofanyika sasa ni kutaka kutuondoa katika hoja, kuna watu wanasema nitafanya mkutano na waandishi wa habari, mimi nikawajibu kuwa hilo haliwezekani. Siwezi kuhama,” amesema.

Akieleza sababu za kusambazwa kwa ujumbe huo amesema, “Wamesambaza uzushi huu baada ya mimi kuandika katika mitandao ya kijamii kuwa unapopigana vita unahitaji jeshi dogo lenye weledi, yaani unaweza kuwa na idadi kubwa ya wanachama lakini wakawa wasaliti.”

Kuhusu gharama za ubunge wake amesema wapo watu waliopigania ushindi awe mwakilishi wao bungeni huku baadhi kupoteza maisha, kufilisika, kufungwa jela na kwamba hawezi kuwasaliti kwa maslahi yake binafsi.

“Thamani ya ubunge haiwezi kushushwa kama vocha ya simu, kwamba ikiisha unaweza kukwangua nyingine,” amesisitiza.

MWANANCHI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527