MAGUFULI ATANGAZA KIMBUNGA KWA WAPINZANI


Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) John Pombe Magufuli ameuambia Mkutano Mkuu wa CCM kuwa kuna idadi kubwa ya wanachama wa vyama vya upinzani ambao wanataka kujiunga na CCM.

Tayari Wabunge wawili wa upinzani, Maulid Mtulia (Kinondoni-CUF) na Godwin Molel (Siha-Chadema) wamejiuzulu nafasi zao na kujiunga CCM.

Akihutubia Mkutano Mkuu wa CCM leo, Jumatatu Desemba 18 Rais Magufuli amesema kuna mbunge mwengine wa upinzani anataka kujiunga na CCM pamoja na madiwani wa kata zake 8. 
“Hiki ni kimbunga, na wataisoma namba," amesema Rais Magufuli.


Magufuli pia amewataka viongozi wa CCM ambao wamechaguliwa hivi karibuni kuhakikisha kuwa jukumu lao la kwanza ni kuongeza idadi ya wanachama, ili ikifika uchaguzi ujao washindani wao wasiambulie chochote.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527