
Mwili wa marehemu ulikutwa nyumbani kwa mganga wa jadi aitwaye Ashura Mkanga mwenye miaka 33 na mkazi wa kitongoji cha Chang’ombe.
Inaelezwa kuwa mazingira ya tukio yanaonesha kuwa mganga huyo wa jadi asiye na kibali kuendesha shughuli za tiba asili analaza wagonjwa nyumbani kwake, anafanya matambiko, anapiga ramli chonganishi, anafanya tohara za watoto katika nyumba yake pamoja na matambiko.
“Tukio hili ni baya na halikubaliki hapa Dodoma na mahala popote, ni fedheha kubwa sana kwa wananchi kuendelea kukumbatia imani za kishirikina katika karne hii na serikali imesogeza huduma za afya karibu na jamii lakini bado wapo watu hawataki kwenda hospitali na kukubali kuuawa kwa fedheha na waganga wachonganishi”, alisema Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa wakati akiongea na waandishi wa habari
Social Plugin