MBUNGE WA CHADEMA ESTER BULAYA AHAMISHIWA BUGANDO

Mbunge wa jimbo la Bunda Mjini, Esther Bulaya aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime alikokimbizwa Jana Jumapili baada ya kuzidiwa akiwa mahabusu ya polisi mjini Tarime, amehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando jjijini Mwanza kwa matibabu zaidi.


Katibu wa Chadema Mkoa wa Mara, Chacha Heche amesema kuhamishiwa Bugando kwa mbunge huyo kumewezekana baada ya kupata dhamana ya polisi aliyowekewa na watu watatu akiwemo wakili wake, Alex Masaba.


Wengine waliomdhamini kwa kusaini hati ya Sh20 milioni ni Mbunge wa Tarime mjini Esther Matiko na Mwenyekiti wa Mtaa wa Songambele ‘B’, Pamba Chacha.


Heche amesema kabla ya kuachiwa kwa dhamana Mkuu wa Wilaya ya Kipolisi (OCD), wa Tarime, Thomas Mapuli alimtembelea mbunge huyo hospitalini kuona hali yake kiafya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post