MBUNGE WA CHADEMA AENDELEA KUSOTA RUMANDE KWA UCHOCHEZI

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Mathias Nyange amesema bado wanaendelea kumshikilia Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga na watamfikisha mahakamani baada ya kukamilisha upelelezi.


Kamanda Nyange amesema sababu za kumtia mbaroni Haonga ni kutokana na kufanya mkutano bila kibali cha polisi katika mji mdogo wa Mlowo-Mbozi na kuwahamasisha wamiliki wa malori na abiria kuandamana kwenda ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, Chiku Galawa.


Amesema Haonga alifanya mkutano huo jana Jumatano, Agosti 2 na alihamasisha madereva wa malori, wamiliki na abiria waende kumuona mkuu wa mkoa.


Amesema lengo la mbunge huyo kuwataka watu hao wamuone mkuu wa mkoa ni kueleza kero yao juu ya adha ya usafiri baada polisi kupitia kitengo cha usalama barabarani kupiga marufuku malori kubeba abiria kutoka katikati ya mji wa Mlowo kwenda maeneo tofauti ya vijijini ambako hakuna usafiri mbadala zaidi ya malori.


“Bado hatujakamilisha upelelezi na tutakapokamilisha muda wowote tutamfikisha mahakamani na kuhusu dhamana tutafikiria kumpatia dhamana ama laa,” amesema Kamanda Nyange.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post