RAIS MAGUFULI AMTEUA MWENYEKITI WA ACT WAZALENDO ALIYEGOMBEA URAIS 2015 KUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 03 Juni, 2017 amemteua Bibi Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.


Bibi Anna Elisha Mghwira anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Saidi Meck Sadiki aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Meja Jenerali Issah Suleiman Nassor kuwa Balozi.

Kabla ya uteuzi huo Meja Jenerali Issah Suleiman Nassor alikuwa Mkuu wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli amemteua DIGP Abdulrahman Omari Juma Kaniki kuwa Balozi.

Kabla ya uteuzi huo DIGP Abdulrahman Omari Juma Kaniki alikuwa Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi.

Tarehe ya kuapishwa kwa wateule wote itatangazwa baadaye.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
03 Juni, 2017

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post