Picha: RAIS MAGUFULI ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA TBC JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo amefanya ziara ya kushtukiza katika makao makuu ya Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) yaliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa ambaye hakutaka jina lake kutajwa alieleza kuwa, Rais Magufuli aliwasili kituoni hapo majira ya saa 5 asubuhi, na miongoni mwa mambo aliyoyafanya ni kusikiliza changamoto zinazowakumba wafanyakazi wa shirika hilo.

“Rais alitembelea hapa majira ya asubuhi na alizungumza na wafanyakazi wa TBC. Ujio wake ulikuwa ni kwa lengo la kujua hasa changamoto tunazokabiliana nazo katika eneo letu la kazi,” kilisema chanzo hicho.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post