TUNDU LISU: HAIJAWAHI KUTOKEA NAFASI YA JAJI MKUU IKAWA WAZI KWA MIEZI 5 TOKEA UHURU

Akiwasilisha bajeti kivuli ya wizara ya katiba na sheria.Mhe.Tundu lissu amesema ni aibu kubwa kama taifa kuwa na mhimili ambao haujakamilika kwa zaidi ya miezi 5
Lissu ametolea mfano mhimili wa serekali na bunge na kusema una viongozi wake.Rais kwa serekali na Spika kwa bunge wapo.

Amehoji iweje mahakama mpaka leo haina jaji mkuu?Amesema ni kumaanisha kuwa ma jaji wa mahakama kuu na rufaa na mawakili nchini wote hawana sifa ya kushika nafasi hiyo?Amesema vipi kuhusu majaji wa jumuiya ya madola?Si wapo kama nchini hamna mwenye sifa?



Amemaliza kwa kusema toka tumepata uhuru hamna rais aliicha mahakama bila jaji mkuu kwa kipindi kirefu kama Magufuli.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527