WANAFUNZI WANNE CHUO KIKUU KIU- DAR WAKIFISHWA MAHAKAMANI KWA KUMKASHFU RAIS MAGUFULI WHATSAPP
Tuesday, February 21, 2017
Wanafunzi wanne wa Chuo Kikuu cha Kampala(KIU) kampasi ya Dar es Salaam, wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, kujibu shitaka la kusambaza picha za kumkashifu Rais John Magufuli kupitia mtandao wa kijamii wa WhatsApp.
Washitakiwa hao ni Amenitha Kongo(19), Maria Tweve (20), Agnes Gabriel(21) na Anne Mwansasu(21), ambapo wamepandishwa mahakamani hapo leo na kusomewa shtaka linalomkabili mbele ya Hakimu Mkazi Catherine Kiyoja.
Kwa pamoja washtakiwa hao wanadaiwa kuchapisha picha ambazo zinaonyesha Rais Magufuli akiwa amevaa hijabu kama mwanamke wa Kiislamu na kuzisambaza kwenye mtandao huo wa WhatsApp, huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.
Washtakiwa wamerudishwa rumande baada ya kushindwa kitimiza masharti ya dhamana.
Chanzo: Mwananchi
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com
Social Plugin