TUNDU LISSU NAYE ATOKA POLISI KWA DHAMANA YA SHILINGI MILIONI 20


Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka manne ya uchochezi.


Wakili wa Serikali Kishenyi Mutalemwa aliwasilisha maombi ya kupinga dhamana yaTundu Lissu kwa madai kwamba amekuwa na mwenendo unaohatarisha amani si tu kwa wanajamii, bali hata kwake mwenyewe kwa kuendelea kutoa maneno ya uchochezi.


Hakimu Huruma Shaidi, ametupilia mbali ombi hilo la serikali na kumpa Tundu Lissu dhamana ya sh. Milioni 20

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post