EZEKIEL WENJE ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI WA CHADEMA KANDA YA ZIWA


Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza, Ezekiel Dibogo Wenje (Chadema 2010/15) amechaguliwa kwenye mkutano mkuu wa Kanda ya Ziwa Victoria, kuwa Mwenyekiti wa Chadema Kanda hiyo. 

Wenje amemshinda Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, Chief Kalumuna ambapo Uchaguzi huo umefanyika hii leo Januari 18,2017 Jijini Mwanza na matokeo yametangazwa hivi punde.

Katika uchaguzi huo, nafasi ya Makamu Mwenyekiti imeenda kwa Ansbert Ngurumo ambapo viongozi mbalimbali wa Chadema Taifa akiwemo Mwenyekiti Freeman Mbowe, wamehudhuria mkutano.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post