Picha: MAZISHI YA PADRE ANDREW LUPONDYA NA WATOTO WATANO WA KAHAMA WALIOFARIKI AJALINI
Thursday, December 29, 2016
Maaskofu wa majimbo manne , mapadri , watawa na mamia ya waamini wameshiriki misa ya mazishi ya Padri Andrew Lupondya (33) na watoto watano wa Shirika Rafiki wa Utoto wa Yesu (VIFRA) na mlezi wao Mama Judith Kajwahula (63 ) wa Jimbo Katoliki Kahama waliofariki katika ajali ya gari.
Ajali hiyo ilitokana na gari walilokuwemo kugongana uso kwa uso na roli aina ya fuso Desemba 24, saa 9 mchana na marehemu walizikwa jana katika eneo la Kiwanja cha Kanisa Kuu la Mtakatifu Karoli Lwanga, Parokia ya Kahama Mjini mkoani Shinyanga.
Misa ya mazishi imefanyika jana katika Kanisa Kuu la Jimbo Katoliki la Kahama na imeongozwa na Askofu Fravian Kasala wa jimbo Katoliki Geita, pamoja na Maaskofu Liberatus Sangu wa Shinyanga, Joseph Mlola wa Kigoma na mwenyeji Askofu Ludovick Minde wa jimbo Katoliki la Kahama.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin