MZEE MWINYI MGENI RASMI SIKUKUU YA EID-EL-ADH-HA SEPT 12,2016
Tuesday, September 06, 2016
RAIS mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Sherehe za Sikukuu ya Eid-El-Adh-ha maarufu kama ‘Eid ya Kuchinja’ itakayofanyika Septemba 12, mwaka huu (Jumatatu ijayo).
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waisalam Tanzania (BAKWATA), Salim Abeid amesema kuwa sikukuu hiyo kitaifa itafanyika jijini Dar es Salaam kwenye Viwanja vya Makao Makuu ya BAKWATA kuanzia saa 1:30 asubuhi huku akiwataka waumini wa dini ya Kiislam kujitokeza kwa wingi.
Katika waraka wake kwa waandishi wa habari, Abeid aliongeza kuwa, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zuber bin Ally anawatakia Waislam wote na wananchi kwa jumla sikukuu njema Sikukuu ya Eid-El-Adh-ha.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin