Makubwa Haya!! MWANAMKE AJIKATA VIUNGO VYA MWILI WAKE NA KUDANGANYA KUWA KAGONGWA NA TRENI ILI ALIPWE

Mwanamke mmoja nchini Vietnam amekiri kutoa mguu na sehemu ya mkono wake vikatwe ili aweze kudai malipo ya bima, kwa mujibu wa polisi.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 30 , anayetambuliwa kama ”Ly Thi N”, alidanganya kuwa aligongwa na treni, limeripoti gazeti la polisi nchini Vietnam.

Lakini kwa sasa ameripotiwa kukiri kwamba alimlipa rafiki yake dola $2,200 (sawa na zaidi ya shilingi milioni 44 za kitanzania) akate viungo vyake.

Lengo lilikuwa ni kudai dola zaidi ya $150,000 (sawa na zaidi shilingi 300,000,000/- za kitanzania) kutoka kwa kampuni ya bima yake.

Kwasasa mwanamke huyo akiwa amepona majeraha yake. anaendesha biashara kwa shida, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527