Kijana Aumwa na Buibui Sehemu Zake Za Siri Akiwa Chooni

Kijana wa miaka 21 mmoja nchini Australia alilazimika kukimbia hospitalini upesi baada ya kuumwa na buibui mwenye sumu kali sehemu za siri.

Mwanamume huyo aliumwa na buibui huyo akitumia choo cha kusafirishwa eneo ambalo kunafanywa ujenzi mjini Sydney.

Aliumwa na buibui aina ya redback katika uume wake. Msemaji wa hospitali ya St George Hospital alithibitisha kwamba  kijana huyo alifika hospitalini na kutibiwa.

Mtu anapoumwa na buibui hupata maumivu makali, kutokwa na jasho na pia kupata kichefuchefu.

Mwanamume huyo baadaye aliruhusiwa kuondoka hospitalini na matabibu wanasema maisha yake hayamo hatarini.

Ingawa kumewahi kuripotiwa visa vya watu kufariki baada ya kuumwa na buibui aina ya redback, hakuna aliyefariki tangu kugunduliwa kwa dawa ya kumaliza sumu mwaka 1956.
 
Via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527