Haya Hapa Matokeo Ya Mechi Za Leo Za Ligi Kuu Soka Tanzania Bara,Msimamo Ulivyo Sasa







Msimamo wa Ligi Kuu Ulivyo kwa sasa


Baada ya malalamiko ya muda mrefu kuhusu klabu ya Dar es Salaam Young Africans kuwa na viporo vingi, hatimae April 16 2016 wamemaliza michezo yao ya viporo kwa ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Yanga walikuwa na michezo ya viporo mitatu na watani zao wa jadi Simba walikuwa wakilalamika Yanga kupendelewa kwa kwa mechi zake kusogezwa mbele, hivyo hawakuwa radhi kuendelea kucheza wakati wakihisi kuna dalili za upangaji wa matokeo.

Mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar hakuwa mwepesi kwa Yanga kwani Mtibwa walionekana kuwa na kikosi kizuri, kitu ambacho kilipelekea dakika 45 za kwanza kumalizika kwa kutofungana, mambo yalibadilika dakika 2 baada ya mchezo kuanza pale winga mshambuliaji wa Yanga Simon Msuva alipoipatia Yanga goli la kuongoza na hatimae mchezo kumalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa goli 1-0.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post