Kali ya Tabora!! MCHUNGAJI WA KANISA ANASWA AKIMHONDOMOLA BINTI WA KAKA YAKE,ALIMTISHA AKIKATAA KUFANYA MAPENZI ATAKUWA KICHAAA



NB-Picha haihusiani na habari hapa chini

Mchungaji wa kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT) katika kijiji cha Mgongoro kata ya Igunga mkoani Tabora, Abel Godfrey, amekamatwa na waumini wake baada ya kudaiwa kukutwa akifanya mapenzi na binti wa kaka yake.



Waumini hao wakishirikiana na uongozi wa serikali ya kijiji hicho, walifanya tukio hilo juzi saa 5:30 usiku akiwa na binti huyo  umri wa miaka 20 jina tunalihifadhi mwenye mtoto mchanga wa miezi minne.


Akizungumza kwa masikitiko babu wa binti huyo, Bictoni Kyarero, alisema mchungaji Godfrey, alikuwa na tabia hiyo kwa mwaka mmoja sasa, lakini tabia hiyo ilimchosha na kutoa taarifa kwa waumini wake pamoja na uongozi wa mtaa kisha kumuwekea mtego uliomnasa akiwa katika nyumba hiyo.


Amesema baada ya kumkamata alijaribu kukimbia lakini walifanikiwa kumdhibiti na kisha kukiri kufanya mapenzi na binti huyo huku akiwabembeleza waumini wake wamfichie siri.


Kwa upande wake binti huyo alipoulizwa kuhusu kufanya uzinzi na baba yake mdogo, alikiri huku akisema alitenda kosa hilo baada ya kutishwa na mchungaji huyo iwapo angekataa angemuombea kwa Mungu ili awe kichaa.


Akizungumzia tukio hilo, mchungaji huyo amekiri kutenda kosa hilo na kubainisha alifanya hivyo baada ya kuzidiwa ‘ujanja’ na shetani huku akitubu na kudai hatorudia tena kosa hilo.


Naye mtendaji wa kijiji hicho, Edward Kitenya, alisema mchungaji huyo walimkamata akiwa katika nyumba ya tembe wakiwa wamelala baada ya kutandika turubai chini wakiendelea kufanya mapenzi na binti huyo kisha kumweka chini ya ulinzi mpaka asubuhi na kupigishwa faini ya Sh. 20,000 na kuachiwa huru.


Kwa upande wao baadhi ya wananchi waliuomba uongozi wa kanisa hilo kumvua uongozi kwa kuwa amekiuka maadili ya uongozi na kufanya waumini kutomwamini tena kama kiongozi wa kiroho.


Mtendaji wa kata ya Igunga, Fredrick Masesa, amewaomba viongozi wa dini pamoja na wananchi kwa ujumla kuzingatia maandiko matakatifu ya mwenyezi Mungu ya kutofanya vitendo viovu ili wamtumikie kiusahihi.


Kwa upande wake mchungaji wa kanisa la kijiji cha Mwanzugi, Fanuel Daniel, alithibitisha kukamatwa kwa mchungaji wa kanisa la kijiji cha Mgongoro, Godfrey na kusema tayari wamemsimamisha kutoa huduma mchungaji huyo kwa muda usiojulikana mpaka uongozi utakapokutana wote kwa ujumla na kuongeza kuanzia sasa kanisa hilo la Mgongoro litaongozwa na Philipo Makeremo ambaye pia ni katibu wa kanisa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527