Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Picha 20!! MDAHALO WA WAGOMBEA UBUNGE JIMBO LA SHINYANGA MJINI LEO..CHADEMA,ACT WAZALENDO,APPT MAENDELEO WAJITAWALA





Leo Jumatano Oktoba 21,2015 kumefanyika mdahalo maalum kwa wagombea ubunge jimbo la Shinyanga mjini mkoani Shinyanga.Mdahalo huo uliofanyika katika ukumbi wa Vijana sente Ngokolo mjini Shinyanga umeandaliwa na Radio Faraja FM Stereo kwa kushirikiana na shirika la AGAPE lengo likiwa ni kuwapa nafasi wagombea ubunge jimbo hilo kueleza kwanini wanagombea nafasi hiyo"Kwa nini wananchi wakuchague wewe kuwa mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini".




Walioshiriki ni Mgombea ubunge kupitia ACT Wazalendo Nyangaki Shilungushela,mgombea wa APPT Maendeleo Emiliana Tambwe,mgombea kupitia Chadema Patrobas Katambi aliwakilishwa na Ntobi Emmanuel wakati mgombea kupitia CCM Stephen Masele hakuonekana wala hakutuma mwakilishi.Washiriki wa mdahalo walizungumzia namna walivyojipanga kuiondoa CCM madarakani na kuboresha maisha ya watanzania,ikiwemo kuleta mabadiliko katika elimu,afya,miundombinu,kilimo,ardhi,viwanda...Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde ametuletea picha 20...kilichojiri ukumbini




Mgombea ubunge jimbo la Shinyanga mjini kupitia chama cha APPT Maendeleo Emiliana Tambwe akizungumza katika mdahalo huo ambapo alieleza wazi wazi kumuunga mkono mgombea urais kupitia Ukawa Edward Lowassa huku akiomba ridhaa kuchaguliwa kuwa mbunge ili kuleta mabadiliko katika sekta ya uchumi,afya,elimu n.k




Mdahalo unaendelea




Mgombea ubunge jimbo la Shinyanga mjini kupitia ACT Wazalendo Nyangaki Shilungushela akinadi sera za chama chake huku akisisitiza kuwa amedhamiria kupitia chama chake kuwaletea maendeleo wakazi wa Shinyanga




Wakazi wa Shinyanga wakiwa ukumbini




Mwakilishi wa mgombea ubunge jimbo la Shinyanga kupitia Chadema Patrobas Katambi,Ntobi Emmanuel akinadi sera za Ukawa/Chadema ambapo alisema lengo la mgombea wake ni kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo la Shinyanga mjini




Wakazi wa Shinyanga mjini wakifuatilia mdahalo




Mdahalo unaendelea


Kushoto ni mtangazaji wa radio Faraja ndugu Simeo Makoba akiongoza mdahalo huku matangazo yakiruka moja kwa moja redioni,kulia kwake ni mtangazaji wa radio faraja bwana Elisha Shambiti



Mdahalo unaendelea




Wananchi wakifuatilia mdahalo




Mwakilishi wa mgombea ubunge jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi,bwana Ntobi Emmanuel ambaye pia anagombea udiwani kata ya Ngokolo akiomba kura kwa wakazi wa Shinyanga ili wamchague Patrobas Katambi ili awe mbunge wao




Mdahalo unaendelea




Mdahalo unaendelea




Mdahalo unaendelea




Mdahalo unaendelea




Wakazi wa Shinyanga wakiwa ukumbini




Mdahalo unaendelea




Mdahalo unaendelea




Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com