![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi8LG4yE98-jXLShFGkmjfLF5kvLGBSm9Jc4VLZomegtGheFQO2Uym2JuMLDrEOmBNU0gmoZtkeqknMKRB6EZGEYcwxoxNHdTL2KR6fVjiCs0XHMHT2AYIT7SYY5w36VlHizC8TUaev9x6S/s640/4.jpg)
Washirikiwa mbio za baiskeli kundi la akina mama wanaoendesha baiskeli wakiwa wamebeba ndoo kichwani wakijiandaa kuanza shindano hilo katika uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga leo wakati wa sherehe za wakulima maarufu Sherehe za Nane Nane zilizohusisha mashindano ya mbio za baiskeli washiriki kutoka kanda ya ziwa yaliyodhaminiwa na kampuni ya bia Tanzania (TBL)kupitia bia yake ya Balimi Extra Lager.Akina mama hao zaidi ya 10 waliendesha walizunguka uwanja wa Kambarage mara 10(Km 4) bila kuanguka wala kuangusha ndoo za maji-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEij_0geEXrtE3NtmnS-W5nFDwWOqo2cm2kv1_WzpGuqwVJeYmt9UzBtO2EWs1E4oIvQL8u2Kds5dhfnhBEUzSiYxkxL8u3m1ieRpIidiqY87eexyxC73OgQ8Iz8zKS8F1TVizN2yBrhAoAM/s640/5.jpg)
Mashindano yakiendelea,ndoo kichwani,speed ya ajabu...
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhuTYDFDyoefH-hp5-e-UG7ZVuZmX4wHmPUZK_FOnHo9Zd_-NRRMpgfzyLiUI7OmbpewYCv4htdoNMUVACoUjwLjPDuH37IFUPhDdY_A5rrcE0BC3a-3YInxw6sIvN5qfyja2MY55ITahGz/s640/6.jpg)
Mshindi wa kwanza Stella Nganga akimaliza mbio hizo .....
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgGmHPv4pAe7uVEr-bson-Ny56E02TvWiGi0qSNpzncTGtnSeNhQi0cPWoGkrAsYDRRoXSqJQDajINBWPtiFgACfbZOZrA6Vx8sXOnN6jWwSLoHKxHP8cCjYvvM8bPnmgPXH4cAoou0SFYy/s640/7.jpg)
Washindi wa kwanza hadi wa tatu mbio za baiskeli za akina mama wakiwa wamebeba ndoo za maji kichwani wakiwa katika picha ya pamoja,kushoto ni mshindi wa kwanza ni Stella Nganga kutoka Maganzo,Shinyanga,katikati ni Christina Richard kutoka Masekelo Shinyanga na Elizabeth Shuli kutoka Lubaga Shinyanga.
ANGALIA HAPA CHINI.VIDEO WANAWAKE WAKIENDESHA BAISKELI WAKIWA NA NDOO ZA MAJI KICHWANI
Video ya Kwanza wanawake wakijiandaa na baiskeli zao
Video ya pili wanawake wakiendesha baiskeli na ndoo za maji kichwani