PROGRAMU YA WINDOWS 10 YAZINDULIWA,MICROSOFT WAMEKUJA NAYO HII


Programu ya Windows 10 imeadhimisha mwanzo mpya katika kompyuta za kibinafsi ,kulingana na mtendaji mkuu wa kampuni ya Microsoft .

Programu hiyo ilizinduliwa kimataifa siku ya Jumatano, na ni jaribio la kampuni hiyo kujaribu bahati yake katika sekta ya simu.

Windows 10 itatolewa bure kwa wateja wengi kama hatua ya kuboresha programu hiyo.

Window 1-10

Hata hivyo makampuni yatalazimka kulipia toleo hilo jipya hivyo watengenezaji wa PC watahitajika kuiweka katika vifaa hivyo.

Wachambuzi wanasema mkakati huo umezinduliwa ili kuharakisha utumizi wake.

Alipofanya mazungumzo ya kipekee na BBC, Satya Nadella alisema ''programu ya windows 10 ni hatua kubwa kwetu sisi kama kampuni, na katika sekta nzima''.



Microsoft imekua mbioni kuizindua kwa muda wa wiki kadhaa zilizopita, hivyo si kila mtu atapata fursa hiyo ya kuboreshewa siku ya kuanzishwa kwake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527