Makubwa haya!! SERIKALI YATANGAZA RATIBA YA KULALA,KUANZIA SASA KILA MTU AWE OFISINI SAA 11 ALFAJIRI BADALA YA SAA 2




Headlines toka Korea Kaskazini sasa hivi ni kwamba hali ya hewa ni joto sana, lakini yapo mengine toka huko ambapo msimu huu wa joto kali umepewa jina la Sambok.

“Ofisi zote, shule, na kila taasisi nchi nzima zinatakiwa kufuata ratiba mpya ambayo Serikali imeweka… Ratiba kwa sasa ni kwamba kila kitu kitaanza kufanya kazi saa 11 asubuhi badala ya saa mbili asubuhi, na mwisho wa shughuli zote ni saa saba mchana” >>>> Hii ni sehemu ya agizo hilo jipya la Serikali ya Korea Kaskazini.

Wastani wa joto la Korea ni kama 29˚ Centrigrade, lakini kwa sasa imefikia mpaka 40˚ Centigrade… Hii sio mara ya kwanza kutangazwa utaratibu huo, wakati Rais Kim Jong-ilakiwa madarakani iliwahi kutangazwa utaratibu wa aina hii pia.

Noma nyingine ni kwamba Maofisini kwenye AC na feni huenda hii isiwe taarifa nzuri kwao, joto limekuwa kali na hakuna maji ya kutosha kwenye vyanzo vya umeme sasahivi, kwa hiyo ishu ya feni na AC kufanya kazi ofisini huenda ikawa kitendawili kigumu kuteguka.

“Kwa maana hiyo wanafunzi watatakiwa kuamka na kuanza kujiandaa saa kumi usiku, hiyo ni ngumu sana na wakati mwingine unakuta watoto wanakosa vipindi viwili au vitatu kila siku” >>>> Huyu ni mmoja wa watu ambao hawajapenda kabisa huu utaratibu.

Watu wengi hawajapenda hiyo ratiba mpya, unaambiwa mpaka Migahawa ya Serikali inatoa huduma mwisho mchana, ukienda jioni au usiku hakuna huduma utakayopata !!

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527